Watoto takriban miya moja wamesaidiwa viombo vya shule yaki dini pa Ubwari some tarafani Fizi.

Published on Tuesday 08 February 2022 - 12:22

Si vous avez aimé cet article, merci de le partager avec vos proches responsables.
Facebook share link Email share link LinkedIn share link Twitter share link Twitter share link Twitter share link Twitter share link

...

Watoto miya moja wame faidika kanzu, kofiya, Jilbabe, Mi'shafu, ma juzu na ma janvi, kutoka kwa Sheikh Qassim Udi, Siku ya ijumapili tarehe 6 february 2022.

Ghafla hiyo imefanyika kunako madrasa tulm'umin inayopatikana katika Kijiji cha Ubwari some, tarafani Fizi, jimboni Kivu ya kusini.

Msaada huo umetolewa naye sheikh Qassim Udi akishirikiana na waalimu wa wili wa masomo hiyo, akiwemo Majaliwa Swedy na Mfaume Furuzi.

Katika maojiano na viombo vya habari, sheikh Qassim Udi, amejulisha kwamba msaada huo umetoka kwa Murat SEVDIGIM akishirikiana naye Umam Demiri kutoka ujerumani.

Msaada huo ni pamoja na kanzu zakiume 50, Kofiya 50, Jilbabe zakike 50, Mis'hafu (Quorani)50, na juzu za quaida 100, pamoja na misala 8.

Kwaupande wake Mwalimu Majaliwa Swedy, ametowa shukrani zake kwa vifao alivio vipokea, nakuendelea kusema kwamba vifao hivio vimekuja kujibu maitaji yao, kulingana na matatizo waliyo kuwa nayo kwenye madrasa tulm'umin.

Mwalimu Majaliwa Swedy ameongeza kusema Mungu awazidishiye walio jitolea kupana msaada huo.

Mutafaamu yakwamba, msaada huo umetolewa kwa watoto, ili dini ya kislam isomeshwe naku iendeleza mbele.

Duru tulizo nazo zatujuza kwamba, msaada huo hautakuwa wa mwisho, bali utaendelea hata Ku vijiji vingine ili dini ya kislam iendeleye.

UDI QASIM


Merci de laisser un commentaire